Rais Samia Suluhu Hassan amezungumza katika Uzinduzi wa Filamu ya Tanzania The Royal Tour Jijini Dar es Salaam na kuchanganua namna uchangiaji wa fedha ulivyokuwa.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Viongozi mbalimbali pamoja na Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa Filamu ya Tanzania The Royal Tour uliofanyika katika Ukumbi wa Julius Nyerere Conventional Centre Jijini Dar es Salaam tarehe 08 Mei, 2022
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu akiwa na Makamu wa Rais Mhe. Philip Isdor Mpango, Rais wa Zanzibar Hussein Ali Mwinyi, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Amos Makalla, Mwenyekiti wa Kamati ya Royal Tour Dkt. Hassan Abbas pamoja na viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi wakitazama Filamu ya Tanzania The Royal Tour katika ukumbi wa Julius Nyerere Conventional Centre tarehe 08 Mei, 2022
Burudani katika Ukumbi wa JNICC katika uzinduzi wa Royal Tour
Wajumbe wa Kamati ya Tanzania The Royal Tour wakifurahia Tuzo yao waliokabidhiwa na Bodi ya Filamu na Shirikisho la Filamu Tanzania kutokana na kazi kubwa waliofanya wakati wa utengenezaji na Utangazaji wa Filamu hiyo ya Tanzania Royal Tour
Mabalozi pamoja na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa pamoja na Wageni mbalimbali wakiwa katika uzinduzi wa Filamu ya Tanzania The Royal Tour katika ukumbi wa Julius Nyerere Conventional Centre tarehe 08 Mei, 2022

Simba yaichapa Ruvu Shooting Kwa Mkapa
Rais Miwnyi atangaza ongezeko la Mishahara