Shirika la Umeme nchini Tanesco limeweka wazi majina na kiasi cha fedha wanachowadai watu mbalimbali waliokuwa wanaiba umeme akiwemo muigizaji maarufu, Wema Sepetu.
Tanesco walifanya ukaguzi wa kushtukiza nyumbani kwa Wema Sepetu na kubaini kuwa alikuwa anatumia umeme kwa njia ya udanganyifu na kutumia umeme bila kulipa.
Kupitia taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana, Tanesco wameonesha kuwa wanamdai Wema Sepetu kiasi cha shilingi milioni 8,200,496.20.