Wizara ya kilimo ya Malawi imemwandikia barua bingwa wa zamani wa ndondi duniani Mike Tyson ikimuomba kuwa balozi wa bangi nchini humo.

Waziri Lobin Lowe amesema kuhalalishwa kwa bangi mnamo 2020 kumeunda fursa kimataifa.

Kwa mujibu wa Vyombo vya habari nchini humo viliripoti kwamba Tyson alitarajiwa nchini Malawi wiki iliyopita lakini ziara yake iliahirishwa.

Wizara hiyo ilisema Jumuiya ya Bangi ya Marekani ilikuwa kuwezesha mpango huo na Tyson.

“Malawi inaweza isijiendeshe peke yake kwani tasnia hii ni ngumu inayohitaji ushirikiano. Kwa hivyo ningependa kukuteua, Bw Mike Tyson, kuwa balozi wa Tawi la Bangi la Malawi,” Bw Lowe aliandika.

Tyson pia ni mjasiriamali na amewekeza katika kilimo cha bangi.

Jay Z ajiandikia rekodi ya kipekee tuzo za Grammy
Young Africans yatii hukumu 'CAS'