Mbunge wa Arusha mjini, Godbless Lema amepinga vikali hotuba iliyokuwa ikisomwa na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi katika hospitali ya mama na mtoto inayojengwa eneo la Burka nje kidogo ya jiji la Arusha.

Hayo yametokea leo Oktoba 18, 2016 ambapo shughuli hiyo ilisimama baada Lema kuvuruga hotuba hiyo na kuipinga vikali akidai imejaa upotoshwaji na siasa ndani yake.

Lema alikuwa akipaza sauti kubwa akisema yeye ndiye aliyetafuta eneo hilo la ujenzi kutoka kampuni ya Mawala Advocate. Bofya hapa kutazama video

Vumbi La Ligi Ya Mabingwa Ulaya Lazidi Kutimka
Video: DC Mjema aibua mazito soko la samaki Feri