Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Kenya, William Ruto na Rais wa zamani wa Liberia, George Weah wamepata ushindi wa tuzo za 12 Viongozi Bora wa Mwaka wa Jarida la Uongozi wa Kiafrika, 2023.

Tuzo hizo, ni kutoka katika vipengele vya Kiongozi wa Usalama wa Mwaka, Mwafrika wa Mwaka, na Kiongozi wa Kisiasa wa Mwaka, mtawalia, kulingana na matokeo ya kura ya mtandaoni ambayo iliona ongezeko la asilimia 29 kwa kura ikilinganishwa na mwaka uliopita.

Tuzo za Watu Bora wa Mwaka za ALM, zinazotambulika kama tuzo kuu za viongozi bora barani Afrika, zinaenzi viongozi ambao wanachangia kwa kiasi kikubwa katika maendeleo ya bara hilo, kubadilisha hadhi yake, na kukuza maendeleo chanya.

Mwenyekiti wa Jarida la Uongozi Afrika, Dkt. Ken Giami, amesisitiza hatua kubwa na michango ya washindi katika Uhai wa Mwamko wa bara la Afrika katika kuendesha maendeleo endelevu, ukuaji wa kiuchumi, na utulivu wa kisiasa.

“Juhudi zao zimeimarisha amani kikanda, zimeboresha huduma za afya na elimu, na zimeunda msingi imara wa utajiri wa kiuchumi na maendeleo ya rasilimali watu katika Afrika,” alisema.

Sherehe rasmi za kutunuku tuzo hizo zimefanyika jioni ya tarehe 15 Machi, Mwaka 2024 kwenye hafla ya kila mwaka ya Tuzo za Watu Bora wa Mwaka za ALM katika Hoteli ya Ethiopian Skylight huko Addis Ababa, Ethiopia, makao makuu ya Umoja wa Afrika.

Akipokea tuzo hiyo, Rais Mstaafu amewashukuru waandaaji wa tuzo hizo na waafrika kwa ujumla na amesema tuzo hiyo ni kwa ajili ya Waafrika wote; viongozi wa kisiasa, wana mageuzi ya kiuchumi, viongozi wa dini, Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Watumishi wa Umma wanaojitoa kwa dhati, wakulima, wafugaji na wananchi wa kawaida wote – ambao wanaamka kila siku kupambania Bara la Afrika kuwa sehemu bora .

Kamati: TBA yatakiwa kuendeleze maeneo yake
Simulizi: Nimethibitisha - ni kweli mapenzi yalizaliwa Tanga