Kufuatia uwepo wa taarifa za visa 19 vilivyothibitishwa katika miji mitano ikiwa ni pamoja na jiji la Brazzaville, Serikali ya Nchi ya Jamhuri ya Kongo imetangaza mlipuko wa ugonjwa wa homa ya Nyani.

Kwa mujibu wa taarifa ya Waziri wa Afya wa nchi hiyo, Gilbert Mokoki amesema licha ya kutangazwa kwa ugonjwa huo bado hakuna vifo vilivyorekodiwa hadi kufikia sasa, huku akiutaka umma kuchukua tahadhari.

Amesema, watu wanatakiwa kutosogeleana na wanaoshukiwa kuambukizwa ugonjwa huo na kuepuka kukaribiana na wanyama au kushika nyama za wanyamapori, huku akisema dalili za ugonjwa huo ni pamoja na homa, maumivu na vidonda kwenye ngozi.

Homa ya Nyani, ni ugonjwa ambao uligunduliwa kwa mara ya kwanza kwa katika nchi jirani ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo – DRC mwaka 1970.

Chama afunguka wanayopitia Msimbazi
Tanzania kuwa na uhakika upatikanaji wa Petroli