Biblia ya Kiebrania ambayo kongwe zaidi duniani – Codex, inatazamiwa kuuzwa kwa mnada baadaye mwaka huu na kwa kiasi cha hadi dola milioni 50 na itakuwa hati muhimu zaidi ya kihistoria kuwahi kuuzwa kwa mnada.

Codex hiyo, inasemekana kuwa ya mwisho wa karne ya tisa au mapema karne ya 10 WK, labda karibu mwaka wa 900 CE. Kipekee kwa nakala ya wakati huu, ina vitabu vyote 24 vya Biblia ya Kiebrania na inakosa “majani” machache tu ya maandishi.

Umri huo, unamaanisha kuwa ni kongwe kuliko Biblia kamili ya mapema zaidi ya Kiebrania, Leningrad Codex, kwa karibu karne moja na imekuwa kwenye kundi la matukio ya kilimwengu kwa karne nyingi ambapo maandishi yanaonyesha jinsi Kodeksi ilivyouzwa na Khalaf ben Abraham kwa Isaac ben Ezekiel al-Attar mwanzoni mwa karne ya 11 WK.

Kufikia karne ya 13, kitabu hicho kiliwekwa wakfu kwa sinagogi la Makisin katika Siria ya leo walakini, mji huo ulifutwa muda mfupi baadaye, ikiwezekana zaidi na Milki ya Mongol katika karne ya 13 au Milki ya Timurid mnamo 1400, na Codex ilitolewa kwa Salama bin Abi al-Fakhr kwa usalama na waliahidi kulirudisha katika sinagogi litakapojengwa upya, lakini wakati huo haukufika.

Karne sita zilizofuata za historia hakukuwa na jambo, lakini baadaye Ciodex iliibuka tena mwaka wa 1929 iliponunuliwa na mkusanyaji Mwingereza, David Solomon Sassoon ambaye alikuwa amekusanya mkusanyo mashuhuri wa kibinafsi wa vitu vya kale vya Kiyahudi ulimwenguni.

Kwa sasa, hati hiyo iko katika mkusanyo wa Jacqui Safra, mwanachama wa familia maarufu ya benki ya Kiyahudi ya Brazili-Syrian-Lebanon. Katika sura inayofuata ya hadithi yake, vizalia hivyo vitauzwa katika mnada ulioandaliwa na Sotheby’s New York mnamo Mei 16.

Uwanja wa Benjamin Mkapa upo hatarini
Mabingwa CECAFA wapongezwa Dodoma