Siku ya Redio Duniani, huadhimishwa kila mwaka ifikapo Februari 13 kuashiria nafasi muhimu ambayo redio inatekeleza wajibu wa kutuhabarisha katika maisha yetu ya kila siku katika jamii.

Siku hii ilianzishwa na Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka 2012, na historia yake ilianza kufuatiliwa kwenye Mkutano wa kwanza wa Kimataifa wa Redio huko Geneva mwaka 1974 na ilitangaza Februari 13 kuwa Siku ya Redio Duniani kwa sababu tarehe hii ndiyo Redio ya Umoja wa Mataifa ilianzishwa kwa mara ya kwanza mwaka 1946.

Kwa kuona umuhimu wa redio, na pia kuhimiza wafanya maamuzi kutoa upatikanaji wa Habari kupitia redio, UNESCO inaratibu shughuli za Siku ya Redio Duniani kwa kiwango cha kimataifa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa, kupitia vituo vyao vya redio.

Kauli mbiu ya Siku ya Redio Duniani 2023 ni ‘Redio na Amani’ ambayo inaangazia jukumu la redio kama chombo huru cha kuleta amani na mada ndogo ya siku hii ni ‘Redio katika Kuzuia Migogoro na Kujenga Amani’ na ‘Msaada kwa Redio Huru’.

Usambazaji wa redio wa kwanza, ulifanywa Mei 13, 1897 na Guglielmo Marconi ambapo matangazo ya kwanza ya redio nchini India yalifanyika mwezi Juni 1923 na Radio Club ya Bombay na sasa India ina karibu vituo 479 vya redio.

Muumini adai zaka Kanisani, asema ameghairi kwenda Mbinguni
GGML wajivunia Nyankumbu Sekondari kung'ara kidato cha nne