Usiku wa kuamkia Desemba 26 2021, kumefanyika muendelezo wa maonyesho kadhaa ya wasanii wanaoliunda kundi la P square, Peter Okoye pamoja na Paul Okoye katika Onyesho lifahamikalo kama ‘PSquare Reactivated’ lililofanyika huko Lagos nchini Nigeria.

Wasanii hao mahiri licha ya kufanya onyesho la kiwango cha juu, waliamua kutumia fursa hiyo ya kukutana na mashabiki zao kuomba msamaha kwa kitendo cha wao kutengana na kutokuwa pamoja kama kundi kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne tangu mwaka 2017.

Sababu za wao kutokua pamoja inasemekana kuchagizwa na maswala ya maslahi ya kikazi huku vyanzo vingine vikidai kuwa ni maswala ya kifamilia yaliyochochewa na wake wa wasanii hao

P Square Reactivated ndio onyesho la kwanza kufanyika tangu wasanii hao walipoungana tena na kuanza kufanya kazi kwa pamoja kama kundi, ambapo sehemu ya kwanza kutumbuiza rasmi ilikuwa Sierra Lione.

Habari kubwa kwenye magazeti leo, Disemba 27, 2021
Zuchu Kinara YouTube