Baada ya kuikanyaga Spurs kwa mabao mawili kwa moja, meneja wa vinara wa ligi ya nchini England (chelsea) Antonio Conte, amewataka mashabiki kuendelea kumpa ushirikiano katika kipindi hiki cha kuelekea mpambano dhidi ya Man city.

Kikosi cha Chelsea kitasafiri hadi Etihad Stadium mwishoni mwa juma hili, kwa lengo la kuzisaka point tatu muhimu mbele ya Pep Guardiola.

Conte amesema mchezo huo utabeba umuhimu mkubwa kwa Chelsea kutokana na umahiri wa kikosi cha wapinzani wao, na anaamini huenda kikawa kipimo tosha kwa wachezaji wa The Blues kwa msimu huu.

Amesema mtihani huo unapaswa kupewa ushirikiano na mashabiki wa Chelsea kwa kuishangilia timu yao ambayo kwa sasa ipo kileleni kwa kufikisha point 31.

“Ni muhimu kwa kila shabiki kutuunga mkono, kutokana na uzito wa mchezo utakaotukabili mwishoni mwa juma hili, ninatarajia kuwaona wakishangilia wakati wote tutakapokua Etihad Stadium,” Alisema Conte.

“Tunapokua Stamford Bridge mashabiki wetu hujivunia kuwa nyumbani, lakini bado wana nafasi ya kuwa nasi hata katika uwanja wa ugenini na tukaonekana tupo nyumbani pia.

“City ni timu nzuri na wanajua nini wanachokihitaji ndani ya dakika 90, lakini juhudi zetu za kuwakabili hazitotosha kama mashabiki hawatokua pamoja nasi,” Alionega meneja huyo kutoka nchini Italia.

Waitara: Makonda toa ushahidi kuhusu tuhuma za Sirro
Sami Khedira Awindwa Marekani