Mahakama kuu kanda ya Arusha  imetengua matokeo ya ushindi yaliyompa ubunge Onesmo  Nangole wa chadema kutokana na udanganyifu

Jaji anayesikiliza kesi hiyo Sivangilwa  Mwangesi amesema ni kutokana na udanganyifu ambapo fomu zilitomika kuandika matokeo ni fomu 21b za udiwani badala ya kutumia  fomu 21c ya ubunge   hivyo uchaguzi utarudiwa

Katika shauri hilo aliyekuwa Mgombea ubunge wa ccm jimbo la longido Dr Steven Kiruswa alipeleka shauri hilo mahakamani dhidi ya mbunge aliyekuwa mbunge wa longido Onesmo ole Nangole

Bw. Nangole ambaye ametenguliwa ubunge leo hii aliwahi kuwa Mwenyekiti wa ccm mkoa wa arusha kabla ya kuhamia chadema agosti 8 2015 .

Video: Mashabiki wa TP Mazembe wakiitambia Yanga, waitangazia magoli 5 kwao
Wananchi waichongea Clouds TV kwa TCRA kwa kurusha 'mada ya ushoga', Makonda awakingia kifua