Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF), Jamal Malinzi amewatumia salamu za pongezi wachezaji Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wanaochezea klabu ya TP Mazembe ya Congo DR kufuatia kutwaa Ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika (CL) jana kwa kuifunga timu ya USM Algiers kwa jumla ya mabao 4-1.

Katika salamu zake kwenda kwa wachezaji hao, Malinzi amewapa hongera kwa mafanikio waliyofikia ya kutwaa ubingwa huo wa vilabu Afrika, na kuwataka waongeze bidii ili waweze kufanya vizuri pia katika michuano ya Kombe la Dunia la Mabara litakalofanyika mwezi Disemba nchini Japan.

Malinzi amesema kwa niaba ya familia ya mpira wa miguu na Watanzania wote wanawashukuru kwa kuiwakilisha vizuri Tanzania kimataifa, na sasa moyo huyo wa kujituma kwao waundeleleze katika mchezo dhidi ya Algeria wikiendi hii kuwania kufuzu kwa fainali za kombe la Dunia 2018 nchini Urusi.

Q Chief Atangaza Ndoa
Malinzi Kuzindua Rasmi Kombe La Shirikisho