Zaidi ya watu arobaini wamefariki dunia na wengine kadhaa wamejeruhiwa, baada ya moto kutokea katika gereza moja kwenye jimbo la Banten Magharibi mwa Indonesia.
Â
Aidha moto huo ambao umezuka alfajiri ya leo Septemba 8, umeteketeza maeneo kadhaa ya jengo la gereza la Tangerang, ambapo baadaye walifanikisha kuuzima.
Â
Jengo hilo la gereza limekuwa likihifadhi wafungwa ambao wanatumikia vifungo mbalimbali, kutokana na makosa yanayoambatana na biashara na matumizi ya dawa za kulevya.
Â
Hata hivyo jengo hilo ambalo lina uwezo wa kuchukua wafungwa 38 limekuwa likichukua wafungwa zaidi ya mara tatu ya uwezo wake, hivyo kusababisha msongamano wa wafungwa.
Â
Wizara ya Sheria na Haki za Binadamu nchini Indonesia imekiri kuwepo kwa msongamano wa wafungwa katika jengo hilo.
Â
Sambamba na hayo yote Uchunguzi unaendelea kuhusu chanzo cha moto huo.