Mwimbaji maarufu mzaliwa wa Marekani, Tina Turner amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 83 baada ya kuugua kwa muda mrefu nyumbani kwake katika mji wa Küsnacht karibu na jiji la Zurich, Uswisi.

Turner ambaye alianza harakati zake za uimbaji miaka ya 1950 wakati muziki aina ya rock ‘n’ roll ulipoanza, aliibuka kwa kasi kiumaarufu na kuwa mahiri katika tasnia hiyo na wimbo wake uliovuma wa “What’s Love Got to Do with It.”

Katika Wimbo huo, aliyaita mapenzi “hisia zilizotumiwa,” na baadaye alijitokeza kama mwanamitindo wa kuigwa katika miaka 1980, alipokuwa akipita katika mitaa ya Jiji la New York akiwa na muonekano wa kipekee.

Aliwahi kupewa jina la utani la “Malkia wa Rock ‘n’ Roll,” na alishinda Tuzo sita kati ya nane za Grammy, katika miaka ya 1980 huku nyimbo zake kadhaa zikiingia kwenye Top 40, zikiwemo “Typical Male,” “The Best,” “Private Dancer” na “Better Be Good To Me.”

Tamasha lake la 1988 mjini Rio de Janeiro, Brazil, lilihudhuriwa na watu 180,000, na linasalia kuwa moja ya kusanyo la hadhira kubwa zaidi kwenye tamasha kwa msanii yeyote kuwahi kutokea.

Tina Turner, alizaliwa huko Anna Mae Bullock Novemba 26, 1939, katika jamii ya vijijini ya Tennessee ya Nutbush, ambayo alielezea katika wimbo wake wa 1973 wa “Nutbush City Limits” kama “jamii ya zamani tulivu ya wakulima.

Watanzania Qatar wahoji kodi, uraia wa watoto wao
Neville, Carragher wataja vikosi EPL 2022/23