Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli amempongeza Rais mteule wa Marekani, Donald Trump kwa ushindi alioupata.
Rais Magufuli pia amewapongeza watu wa Marekani kwa ujumla kwa kuendesha uchaguzi wa kidemokrasia.
Kupitia ujumbe huo alioweka katika akaunti yake ya Twitter, Rais Magufuli amemhakikishia kuendeleza urafiki kati ya mataifa hayo mawili