Bodi ya wadhamini ya Chama cha Wananchi (CUF) imekata shauli mahakama kuu dhidi ya Prof. Lipumba, wanachama kumi na mbili wa chama hicho na Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, Jaji Francis Mutungi.
Hayo yamesemwa leo Oktoba 5, 2016 na Wakili wa CUF, Nassor Juma ambapo ameeleza kuwa bodi hiyo imefungua shauri Mahakama Kuu ikitaka kupata amri ya Mahakama ili kumzuia Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kufanya shughuli za kisiasa nje ya mamlaka aliyopewa na sheria na kanuni za vyama. Bofya hapa kutazama video