Macho yote yameelekezwa mji wa Abuja nchini Nigeria ambapo baadaye leo wachezaji bora wa soka kutoka Afrika 2015 watatangazwa.

Makala ya 24 ya Tuzo hizo za Glo-CAF, zinazotolewa na Shirikisho la soka barani Afrika (CAF), yamekuwa na ushindani mkali kutoka kwa wachezaji wa soka wanaosakata soka ya kulipwa ndani na nje ya Afrika.

 

Orodha ndefu iliyowasilishwa mwezi Oktoba mwaka uliopita, ilipunguzwa hadi wachezaji watatu kila kitengo.

Mchezaji Bora Afrika

Andre Ayew (Ghana/ Swansea City)

Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon/Borussia Dortmund)

Yaya Toure (Cote d”Ivoire/ Manchester City)

Mchezaji bora anayechea soka barani Afrika

Baghdad Boundjah (Algeria/: Etoile du Sahel)

Mbwana Aly Samata (Tanzania/ TP Mazembe)

Robert Kidiaba (DR Congo/ TP Mazembe)

Matumaini ya Afrika mashariki yamo kwenye kitengo cha tuzo ya mchezaji bora anayechea soka barani Afrika ambapo mshambuliaji Mbwana Aly Samatta wa Tanzania na klabu ya TP Mazembe yumo ndani.

Nyota huyo aliyeisaidia klabu ya Mazembe kuondoka na kombe la klabu bingwa afrika, atakuwa anawania taji hilo dhidi ya mdakaji wa klabu yake ya Mazembe, Robert Kidiaba ambaye pia ni kipa wa DR Congo na raia wa Algeria Baghdad Bounedjah anayeichezea Etoile du Sahel.

Samatta aliibuka mfungaji mabao bora Ligi ya Klabu Bingwa Afrika mwaka uliopita.

Katika kitengo cha Tuzo ya Mchezaji Bora Afrika kinachoshirikisha wachezaji wa ligi za nje, Yaya Toure, aliyeshinda tuzo hiyo mara nne awali, ni mmoja wa wanaoipigania.

Toure, ambaye ni kiungo wa Ivory Coast na Manchester City anakabiliwa na upinzani kutoka kwa mshambuliaji wa Gabon na klabu ya Borrussia Dortmund Pierre-Emerick Aubameyang, na Andrew Ayew kutoka Ghana na Swansea City.

Tangu kuanzishwa kwa tuzo hizo 1992, ni wachezaji kumi na wanne pekee wakiwemo Yaya Toure na Didier Drogba ambao wametuzwa.

IAAF Yamfungia Maisha Papa Massata Diack
Kaijage Wa Twiga Stars Atangaza Kujiweka Pembeni