Watu wanne wanashikiliwa na polisi nchini Nigeria kwa kudaiwa kuuza na kula nyama za binaadamu.

Kamishna wa polisi katika jimbo la Zamfara kaskazini-magharibi mwa Nigeria, Elkanah Ayuba, alisema kuwa wanne hao walikamatwa baada ya maafisa wa upelelezi waliokuwa katika harakati za kufanya uchunguzi wa kupotea kwa mvulana wa miaka tisa, kupata maiti katika jengo ambalo halijakamilika huku baadhi ya sehemu za mwili zikiwa zimetolewa.

Kamishna huyo pia alisema vikosi vya usalama vimewaokoa watu 17 waliotekwa nyara katika jimbo jirani la Niger na kupelekwa Zamfara na washukiwa hao ni wanaume wawili na wavulana wawili huku washukiwa wengine wa genge hilo wakisakwa.

Ayuba amesema vikosi vya usalama vilivyokuwa kwenye doria pia vimefanikiwa kupata baadhi ya silaha ikiwa ni pamoja na vifaa vya kurusha roketi kutoka kwa genge moja baada ya makabiliano ya risasi karibu na msitu.

Siku ya Ijumaa hapo iliripotiwa kuwa zaidi ya watu 100 waliuawa na watu wanaoshukiwa kuwa ni majambazi katika eneo hilo, baada ya watu 300 waliokuwa na pikipiki kufika katika jamii kama tisa kati ya Jumanne na Alhamisi usiku.

Mnamo Juni, watekaji nyara walichukua wanafunzi 102 na walimu wanane kutoka shule moja katika jiji la Birnin Kebbi. Nambari ambayo haikutajwa tayari ilikuwa imeachiliwa mwaka jana, baada ya wazazi wao kufanya mazungumzo na watekaji.

Utekaji nyara kwa ajili ya fidia ni biashara kubwa ya uhalifu nchini Nigeria ambapo Simulizi iliyovuma wikendi hii kuhusu baba kutoka jimbo la Katsina, linalopakana na Zamfara mashariki, ambaye amekuwa akiondoa paa la nyumba yake ili kuuza mabati hayo ili kupata fidia ya takriban $250 (£180) kwa mwanawe.

Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari ameahidi kuwa serikali haitalegea katika vita vyake na “waharamia”.

“Mashambulizi ya hivi karibuni dhidi ya watu wasio na hatia ni kitendo cha kusikitisha sana ,, sasa chini ya shinikizo kubwa kutoka kwa vikosi vyetu vya kijeshi,” alisema katika taarifa yake Jumamosi usiku.

Vikosi vya jeshi la Nigeria vilisema wiki hii kwamba vimewaua “majambazi wenye silaha na wahalifu wengine 537” katika eneo hilo na kuwakamata wengine 374 tangu Mei mwaka jana.

Hivi karibuni takriban watu 200 katika jimbo la Zamfara kaskazini-magharibi mwa Nigeria wamezikwa baada ya wimbi la mashambulizi makali ya magenge ya watu wenye silaha kwa siku kadhaa.

Picha ya Nyani aliyechunwa ngozi yamponza Kanye West
Wasioamini Mungu kushtaki nyumba za ibada