Rais wa Marekani Joe Biden amesema ataviondoa vikosi vyote vya majeshi ya Marekani nchini Afghanistan, kabla ya kumbukumbu ya miaka 20 za mashambulizi ya Septemba 11.

Hatua hii itakuwa imefikisha mwisho vita vilivyoihusisha Marekani kwa muda mrefu zaidi, licha ya hofu ya ushindi wa Taliban.

Kwa wiki kadhaa sasa, Rais Biden amekuwa akionyesha ishara kwamba atauacha muda wa mwisho wa mwezi Mei, wa kuviondoa vikosi vya Marekani nchini Afghanistan, uliowekwa na mtangulizi wake Donald Trump upite.

Maafisa katika Wizara ya Ulinzi ya Marekani walikuwa wanaipinga tarehe ya mwisho ya kuondoa majeshi ya Mei Mosi, wakisema jambo hilo linastahili kufanyika kwa kuzingatia hali ya amani Afghanistan yakiwemo mashambulizi ya Taliban.

Rais wa Somalia asaini sheria ya kuongeza muda wa kukaa madarakani
Mama wa kambo wa Obama afariki dunia