Rais wa Marekani, Joe Biden ameahidi kuunga mkono uchunguzi kuhusu kombora lililoua raia wawili wa Poland katika mlipuko, na kusema kombora hilo pengine halijarushwa kutoka nchini Urusi.

Maoni ya Biden yanakuja baada ya Poland kufanya mkutano wa dharura wa baraza lake la usalama na ulinzi wa taifa baada ya tangazo la Rais wa Poland, Andrzej Duda, kwamba kuna uwezekano angetaka kutumia Kifungu cha 4 cha katiba ya NATO, la usalama wa taifa kuitishiwa.

Ukaguzi mara baada ya mlipuko uliosababisha vifo vya watu wawili nchini Poland. Picha ya The Times of Israel.

Kremlin, imekana kuhusika na mlipuko huo, na hakuna ushahidi uliojitokeza kwamba mgomo huo ulikuwa wa makusudi, au kwamba Urusi ilihusika licha ya kwamba ilishambulia miundombinu ya umeme ya Ukraine, katika mojawapo ya mashambulizi makubwa zaidi ya angani tangu uvamizi huo uanze.

Wanadiplomasia wawili kutoka nchi za NATO, wamesema kuwa mabalozi wa NATO watakutana mjini Brussels hii Novemba 16, 2022 kujadili hali hiyo, huku Rais Biden akiungana na viongozi wa G7 kujadili hali ya Poland.

Mangungu achimbwa mkwara Simba SC
Wadau wataka elimu ongezeko wagonjwa wa Kisukari