Mbunge wa Bumbuli, January Makamba amesema kifo cha Rais wa Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ahayati Dkt. John Magufuli kimeleta kipindi cha mpito chenye wasiwasi lakini Rais Samia Suluhu ameanza vizuri kuendeleza yale aliyoacha Rais na kufanya marekebisho na mashahihisho pale panapostahili.

Makamba ameongea kauli za kutiliana shaka, utengano, kuhukumiana na tuhumiana hazijengi na zinawachanganya wananchi.

“Kaendelea kusema pia mazuri aliyofanya Rais Magufuli hayatapotea kwa kauli za kubeza lakini pia wanaotoa maoni ya kurekebisha mambo wasionekane ni wasaliti kwani ameanza kuona dalili ambazo sio nzuri,” amesema Makamba.

Balozi Mulamula aanza kazi rasmi
Balozi Mulamula akoshwa na utendaji wa Kabudi