Ommy Dimpoz amekuwa miongozi mwa wasanii wachache nchini walioamua kuitumia fursa ya kilimo baada ya kutambua kuwa licha ya kuwa ni uti wa mgongo wa uchumi wetu, ni eneo linalouleta utajiri kwa karibu sana.
Wiki iliyopita, mwimbaji huyo alipost kwenye Instagram picha inayomuonesha akiwa katika eneo lake la shamba analolimiliki nje ya jiji la Dar es Salaa na kuandika, “Shamba Day”.
Wasanii wengine wanajihusisha na Kilimo ni pamoja na Masanja Mkandamizaji, Ditto na wengine wengi.