Nchini Kenya yamefanyika maonyesho ya urembo kwa watu wanaoishi na ulemavu wa ngozi. Mashindano hayo yamefanyika jijini Nairobi Kenya Oktoba 21, 2016 ambapo mamia walijitokeza kushuhudia maonyesho hayo yaliyovutia sana kwa kila aliyeshuhudia.
Katika maonyesho hayo, mrembo Louise Lihanda ambaye ni mwanafunzi alitangazwa kuwa mshindi wa kwanza wa taji hilo la urembo katika mashindano hayo huku Jairus Ongetta akikabidhiwa taji la uanamitindo bora kwa wanaume.
Â
Mrembo, Louise Lihanda aliyeshinda taji la urembo kwa akina dada akitembea jukwani akiwa amevalia vazi la kupendeza lililotengenezwa kwa kutumia puto.
Wanaume walioshiriki katika mashindano hayo ya urembo kwa watu wanaoishi na ulemavu wa ngozi ama Albinos jijini Nairobi, Kenya. Tarehe 21 Oktoba 2016.
 Jairus Ongetta, ambaye amekabidhiwa taji ya uanamitindo bora kwa wanaume akiwa jukwaani na mavazi ya kupendeza.
Erick Thomas, awaongoza wanamitindo wenzake kwenye jukwaa wakati wa mashindano ya urembo kwa watu wanaoishi na ulemavu wa ngozi. Lengo lake ni kuhakikisha kwamba watu walio na ulemavu huo wamejivunia ngozi yao.
Msichana nayeishi na ulemavu wa ngozi akitazama maonyesho hayo, Yeye ni miongoni mwa watu ambao kila siku wanakabiliwa na hatari ya kuwawa kutokana na imani za kishirikiana Afrika mashariki na Afrika kusini.
John Ngatia, ambaye pia huwa anasakata densi, avalia sare ya mapigano ya ndondi katika maonyesho hayo, jijini Nairobi Kenya tarehe 21 Oktoba 2016
Majaji wakiwa makini kufuatilia shindano, waaliongozwa na mwanamitindo wa kimataifa Deliah Ipupa (katikati) tarehe 21Oktoba 2016.
Naomi Wafula, akiwa amevalia vazi lililotengenezwa kwa sahani za plastiki katika mashindano ya urembo yaliyofanyika jijini Nairobi, Kenya tarehe 21 Oktoba 2016
Mamia walihudhuria maonyesho hayo kuonyesha umoja wao na watu wanaoishi na ulemavu wa ngozi katika mkahawa wa Carnivore jijini Nairobi Kenya, tarehe 21, Oktoba 2016
Amina Makokha akiwa amevalia sare ya mchezo wa raga katika mashindano ya urembo yaliyofanyika jijini Nairobi, Kenya tarehe 21 Oktoba 2016
Kutoka kulia, Naibu rais wa Kenya William Ruto, Mbunge Isaack Mwaura na mkurugenzi mkuu wa bodi ya filamu nchini Kenya Ezekiel Mutua pia walikuwemo.