Wafanyakazi wa kujitolea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameingia mtaani kuimba na kucheza wakijaribu kuleta furaha kwa maelfu ya watoto waliokimbia makazi yao, kutokana na ghasia huku wengine wakiishi katika mazingira hatarishi kwenye kambi zilizoboreshwa za watu walioyamaha makazi yao katika mkoa wa Nyiragongo.

Wanachama wa kikundi cha Goma Actif, kinachowaleta pamoja wasanii, wanamuziki, wafanyabiashara na wakazi wengine wa Goma kusaidia wale wanaohitaji, kuandaa chakula cha kugawiwa miongoni mwa familia zinazokimbia vita kati ya Jeshi na waasi wa M23 pia wameshiriki zoezi hilo la kurejesha matumaini kwa watoto.

Wanachama Goma, wakigawa chakula kwa watoto.

Wakihojiwa wakati wa tukio hilo baadhi yao wamesema, “Tunakuja kila asubuhi kutoa uji na mikate kwa watoto kati ya elfu 2 na elfu 5 kulingana na siku, ili kuondoa picha za madhara ya kibinadamu kwa watoto ya kuanzishwa tena kwa mapigano kati ya Jeshi la Kongo (FARDC) na M23 katika eneo la Rutshuru.

Mapigano katika maeneo hayo, pia yamehusishwa na ukandamizaji wa haki za raia, ambapo Umoja wa Mataifa kupitia taarifa yake ulisema kuwa watu 188,000 wameyakimbia makazi yao tangu mapigano yalipoanza tena Oktoba 20, 2022 na kufanya idadi ya watu waliokimbia makazi yao kufikia angalau 237,000 tangu Machi wakati mapigano ya kwanza yalipozuka.

Watoto wakisubiri kupatiwa uji huko DRC.

Inaarifiwa kuwa, Takriban asilimia 60 ya waliokimbia makazi yao ni watoto (chini ya umri wa miaka 18). Zaidi ya watoto 76,000 wamekatizwa masomo yao huku watoto 2,000 wakifaidika na programu ya kisaikolojia na vikao vya uhamasishaji vinaandaliwa ili kupunguza hatari za unyanyasaji wa kijinsia, unyanyasaji wa kijinsia na unyonyaji, wakati huduma kwa wahasiriwa inaanzishwa.

Hata hivyo, hali katika Kivu Kaskazini ni ngumu na inazidi kuzorota kutokana na binadamu kukabiliwa na hatari za uwepo wa magonjwa, njaa na hata kukosa maeneo ya kuishi na uhakika wa salama ya maisha yao kutokana na mapigano yanayoendelea huku majimbo ya Ituri na Kivu Kaskazini yakiwa na asilimia 64 ya wakimbizi na watu milioni 5.7.

Rais Samia afafanua tozo Daraja la Kigamboni
Ongezeko bajeti sekta ya uvuvi kuinua pato la Taifa