Uchunguzi wa ndani wa Bunge umependekeza vikwazo dhidi ya wafanyakazi wanaoaminika kuvujisha taarifa kuhusu ununuzi wa magari mawili ya kifahari ya Shilingi 2.4 bilioni kwa ajili ya matumizi ya usafiri wa Spika, Anita Annet Among na Naibu wake Thomas Tayebwa.

Ripoti ya uchunguzi wa siri, ya Idara ya Bunge ya Uchunguzi wa Jinai iliyotayarishwa kwa Tume ya Bunge kitengo cha usimamizi cha Bunge, ilipendekeza kuidhinishwa kwa ufuatiliaji juu ya mfanyakazi mmoja wa karibu wa watu wengine wawili ili kubaini kama walihusika.

Gari la Spika lililoleta utata wa kiasi kikubwa cha manunuzi shilingi 2.4 bilioni nchini Uganda.

“Kuzingatia maoni haya bila shaka kutapunguza mazoea mabaya ya kushiriki hati za siri kwa watu ambao hawajaidhinishwa bila kuadhibiwa,” ilisema ripoti hiyo iliyotiwa saini na naibu mkuu wa CID wa bunge, Charles Twiine.

Timu ya Twiine, ilianza uchunguzi wa kesi hiyo Juni 13 kufuatia malalamiko ya Karani wa Bunge, Adolf Mwesige, kudai kufichuliwa kwa maelezo ya manunuzi ya gari ya Spika kwenye mitandao ya kijamii na mwanahabari Agather Atuhaire mwezi Aprili.

Bunge la Jamhuri ya Uganda.

Bado haijulikani ikiwa tume ilitekeleza mapendekezo hayo, lakini Sheria ya Ulinzi ya Wafichuaji wa taarifa ya mwaka 2010 inawabeba watu katika sekta ya kibinafsi na ya ile ya umma juu ya kufichua habari yenye maslahi ya umma ambayo inahusiana na vitendo visivyo vya kawaida, haramu au ufisadi.

Hata hivyo, Sheria hiyo pia inatoa ulinzi dhidi ya unyanyasaji wa watu wanaotoa ufichuzi, na mambo mengine yanayohusiana juu ya arifu za Habari zenye maslahi kwa umma.

Uwasilishaji mapendekezo sheria ya Habari waendelea
Polisi watatu wakutwa na hatia mauaji ya Wakili