Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad amemuandikia barua kiongozi mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis akimuomba kuingilia kati kwa kutumia ushawishi wake kutatua mgogoro wa Zanzibar kwa amani.

Barua hiyo imebainika kuwa iliandikwa Novemba 25 mwaka jana, ambapo Maalim Seif alimuelezea papa Francis kuhusu hali ya kisiasa nchini Zanzibar na kinachoendelea kuwa kinaweza kupelekea hali mbaya.

“Ni wiki tatu sasa tangu kufanyika kwa uchaguzi mkuu na hali hii imesababisha kusimama kwa baadhi ya shughuli za kuichumi kutokana na wananchi wengi kuwa na hofu kuhusu mustakabali wa hali hii….watu wanashindwa kujua nini kitatokea maana wana hofu kwamba hali hii inaweza kuharibu umoja wa kitaifa kwa watu kuishi kwa upendo bila kujali dini wala kabila,” Maalim seif aliandika.

Maalim Seif ambaye pia ni Makamu wa kwanza wa rais wa Zanzibar, alimueleza Papa Francis kuwa Zanzibar ni nchi yenye mchanganyiko wa madhehebu mbalimbali ikiwa ni pamoja na waislamu na wakristo wanaoishi kwa amani na utulivu siku zote bila kuwa na hofu.

Alisema kuwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeungana na wenzao wa Zanzibar kuwatishia wananchi badala ya kukemea na kuchukua hatua dhidi ya kile alichokiita uovu dhidi ya katiba.

Alimueleza Papa Francis kuwa hatua ya wananchi kutopewa haki yao ya kuchagua kupitia kisanduku ikiwa ni baada ya miaka 20, kunaweza kupelekea vijana ambao hawafurahishwi na mwenendo huo, kuamua kutumia njia mbaya kutafuta haki yao.

“Badala ya kuchukua hatua za pamoja kuzuia uovu huu, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo chama chake kilishinda kwenye uchaguzi mkuu uliopita, imekuwa ikisaidia serikali ya Zanzibar kwa kutumia askari na majeshi yake  kutishia watu wa upinzani,”ilisema.
“Wakati mmishenari wa kikristu alipomuomba Sultan  wa Zanzibar  mwaka  1840  kibali cha  kujenga asasi ya kusaidia jamii kwenye eneo lake, Sultani yule ambaye alikuwa Muislamu alimtambua kama mtumishi wa Mungu aliyekuwa na lengo la kuendeleza neno la Mungu” aliandika.

Nape awataka Chadema wamtimue Lowassa
Magaidi Waishambulia Indonesia, saba wapoteza maisha