Mwanamuziki nguli wa dansi nchini, Kassim Mapili amefariki dunia.

Mwanamuziki huyo aliyetamba na bendi za Shikamoo Jazz na Polisi Jazz, amefia nyumbani kwake maeneo ya TIOT Tabata.

Mapili alihudhuria mazishi ya mwandishi Fred Mosha.

Marehemu alifariki ndani kwake akiwa amelala na hakuna aliyejua mpaka jioni hii majirani walipoingia kutokana na kutoonekana kwake kwa siku tatu. Wakachungulia ndani na kuuona mwili.

Polisi wakataarifiwa na kufika na kuvunja mlango na kuutoa mwili wa marehemu!

Inna Lillahi wa inna ilaihi raji’un!

Hadji Manara: TFF Msipioamua, Tutaamua Sisi
Alex McLeish Kocha Mpya Zamalek FC