Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa ametoa taarifa ya mwenendo wa Ugonjwa wa Corona nchini ambapo amesema kuwa kuna maambukizi mapya ya ugonjwa huo kwa watanzania 196 .

Majaliwa amesema walioambukizwa kutoka Bara ni 174, Zanzibar 22 na kufanya jumla ya watu waliopata maambukizi kuwa ni 480.

Aidha,waziri Majaliwa amesema kuwa idadi ya wagonjwa waliopona imeongezeka kutoka 48 hadi kufikia 167, (Zanzibar wako 36, Bara ni 83).

Katika taarifa hiyo, ameeleza kuwa vifo 6 vimetokea na kufanya jumla ya waliofariki kwa ugonjwa wa Corona kufikia 16 hadi sasa.

Waziri Mkuu ametoa rai kwa Watanzania kuacha kutoa taarifa za uzushi za vifo kuwa kila Kifo kinachotokea hakisababishwi na Ugonjwa wa Corona.

Tanzia: Mkuu wa uhamiaji Kagera afariki Dunia
Kitendawili cha kuendelea ligi kuu, TPLB waitupia mpira TFF